TEHRAN, IRAN
Kitengo cha Uhusiano wa Umma cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) kimetangaza kuanza kwa operesheni kabambe ya kijeshi iitwayo “Nasr” dhidi ya maeneo nyeti ya kijeshi ya utawala wa Israel.

Operesheni hiyo, ambayo imezinduliwa rasmi kwa kaulimbiu takatifu ya “Ya Haidar Karrar”, imelenga kambi za anga za kimkakati za Nevatim na Tel Nof. Kwa mujibu wa taarifa ya IRGC, shambulio hili ni maalum kwa ajili ya kuenzi mashahidi wa vita vya siku 12 na ni jibu la moja kwa moja kwa uchokozi wa hivi karibuni wa makombora uliofanywa na “utawala wa Kizayuni” dhidi ya vituo vya rada nchini Iran.

Jeshi hilo limebainisha kuwa kasi ya utekelezaji na upana wa orodha ya maeneo yaliyolengwa ni sehemu ya mikakati iliyopangwa kwa umakini mkubwa katika hatua hii.

Aidha, IRGC imetoa onyo kali ikisema kuwa vitengo vyote vya mapigano viko katika hali ya juu ya tahadhari na vimejipanga kikamilifu kutekeleza operesheni kubwa zaidi katika nyanja zote, kulingana na hatua yoyote itakayochukuliwa na adui. Duniani kote, macho na masikio yameelekezwa katika eneo hilo kufuatia kuanza kwa operesheni hii ambayo Iran imeitaja kuwa ni “fundisho” kwa adui zake.

Leave a Reply