TEL AVIV, ISRAEL
Balozi wa Marekani nchini Israel ametoa taswira ya hofu na taharuki inayotanda nchini humo kufuatia mashambulizi makali ya makombora yanayoendelea kurindima katika maeneo mbalimbali.

Kupitia ujumbe wa dharura aliochapisha katika mtandao wa kijamii wa X (zamani Twitter), mwanadiplomasia huyo wa juu amethibitisha kuwa amelazimika kukimbilia kwenye vyumba maalum vya usalama vya chini ya ardhi (shelters) ili kujiokoa.

“Kwa sasa niko mafichoni. Nasikia sauti za milipuko mikubwa na ya kutisha ikivuruma juu yangu,” aliandika Balozi huyo, akielezea hali ya hatari inayoshuhudiwa wakati huu.

Ujumbe huo umekuja wakati anga la Israel likiwa limetawaliwa na vishindo vya milipuko inayotokana na makombora yanayopita, huku ving’ora vya tahadhari vikiendelea kulia mfululizo. Kauli hii ya Balozi inasisitiza ukubwa wa mashambulizi hayo ambayo yamezifanya mamlaka zote na raia nchini humo kuwa katika hali ya juu ya tahadhari.

Leave a Reply