TEL AVIV – Vyanzo vya habari kutoka ndani ya Israel vimeripoti kutokea kwa shambulio kubwa la makombora lililofanywa kwa ushirikiano kati ya nchi za Iran na Yemen dhidi ya maeneo yanayokaliwa kwa mabavu na utawala huo.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo vya Kiebrania, operesheni hiyo ya pamoja imelenga maeneo muhimu, jambo lililosababisha mamlaka za ulinzi wa ndani za utawala wa Kizayuni kutoa amri ya dharura. Wakazi na walowezi wa maeneo ya katikati mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu wametakiwa kukimbilia mara moja kwenye maficho ya chini ya ardhi (shelters) ili kujiokoa na mashambulizi hayo.
Hali ya usalama imezidi kuwa tete huku ving’ora vya hatari vikiripotiwa kulia katika miji mbalimbali, ikiashiria ukubwa wa shambulio hilo la pande mbili ambalo limezua hofu kubwa miongoni mwa raia.