Mjumbe wa chama cha Democratic katika Baraza la Wawakilishi la Marekani, Jason Crow, amesema kuwa vita vilivyoanzishwa na Rais Donald Trump dhidi ya Iran vimekuwa janga kubwa lenye gharama kubwa.Akihoji sera hiyo, Crow alieleza kuwa hadi sasa jumla ya dola bilioni 100 zimetumika katika mzozo huo, bila mafanikio ya wazi.Aidha, alisisitiza kuwa hakuna ushahidi uliowasilishwa unaoonyesha kuwepo kwa tishio la haraka kutoka Iran. Kwa mujibu wake, juhudi za kuthibitisha madai hayo zimeachwa, kwani hakuna ushahidi wa kuunga mkono hoja hizo.Aliongeza kuwa hali hiyo inaibua maswali makubwa kuhusu msingi na uhalali wa hatua zilizochukuliwa.