Tehran — Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) limeonesha hadharani boti mpya ya mashambulizi ya kasi yenye silaha za makombora, inayojulikana kwa jina la “27 Rajab.”

Boti hiyo yenye mwonekano wa chini na muundo wa kisasa, unaodhaniwa kuwa wa aina ya trimaran au catamaran, imeripotiwa kuwa na uwezo wa kubeba makombora mawili ya cruise yenye masafa ya hadi kilomita 700. Aidha, chombo hicho kinadaiwa kuwa na uwezo wa kufanya kazi katika mawimbi yenye urefu wa hadi mita 3.

Hatua hiyo inaonekana kuendana na mkakati wa muda mrefu wa Iran wa kutumia kile kinachoitwa “mosquito fleet”, yaani kundi la boti ndogo, za gharama nafuu na zenye mwendo wa kasi, zinazoweza kutumika kwa mashambulizi ya pamoja dhidi ya meli kubwa za kijeshi.

Wachambuzi wa masuala ya usalama wanaeleza kuwa mbinu hiyo inalenga kuongeza uwezo wa Iran wa kutoa tishio kwa meli za kivita katika Ghuba ya Uajemi na Mlango wa Hormuz, maeneo yenye umuhimu mkubwa kwa usafirishaji wa nishati na usalama wa baharini.

Kuzinduliwa kwa boti hiyo mpya kunatajwa kuwa sehemu ya juhudi za Iran za kuimarisha uwezo wake wa kijeshi wa majini katika kipindi ambacho mvutano wa kikanda unaendelea kushuhudiwa Mashariki ya Kati.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *