Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman amesema kuwa mazungumzo aliyofanya na mwenzake wa Iran kuhusu Mlango wa Hormuz yalikuwa na tija.Ameeleza kuwa kuna umuhimu wa kuimarisha juhudi za kidiplomasia pamoja na kutafuta suluhisho za vitendo ili kuhakikisha uhuru wa urambazaji – mchakato wa kuelekeza na kusimamia mwendo wa chombo cha usafiri kama meli, ndege, au hata gari kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa usalama na ufanisi – katika eneo hilo unadumishwa kwa muda mrefu.