Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, ameonya kuhusu uwezekano wa hatua za kijeshi dhidi ya Iran, akisisitiza kuwa vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo viko tayari kujibu kwa nguvu dhidi ya aina yoyote ya uchokozi.

Katika kauli yake, Ghalibaf amesema kuwa “mikakati na maamuzi mabaya huzaa matokeo mabaya,” akiongeza kuwa dunia tayari imejifunza kutokana na uzoefu uliopita.

Aidha, amesema Iran ipo tayari kukabiliana na hali yoyote inayoweza kujitokeza, huku akidai kuwa “watashangazwa” na majibu ya nchi hiyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *