Rais wa Marekani Donald Trump amesema amezungumza na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuhusu majibu ya hivi karibuni ya Iran katika mazungumzo yanayoendelea kuhusu mgogoro huo.

Trump alielezea mazungumzo yao kama “simu nzuri sana” na kusema kuwa Marekani ina uhusiano mzuri na Israel.Akizungumza kuhusu majibu ya Tehran, Trump alisema amekataa pendekezo jipya la Iran lililolenga kumaliza vita. Katika mahojiano na Axios, alisema haridhishwi na barua iliyotumwa na Iran, akisema kuwa haifai na kwamba hapendi majibu yao.

Trump pia alitoa kauli kali dhidi ya Iran, akidai kuwa kwa muda wa miaka 47 nchi hiyo imekuwa ikitumia mbinu za udanganyifu dhidi ya mataifa mengi.

Kauli hizo zinakuja baada ya Washington kusubiri kwa siku 10 kupokea majibu ya Tehran, huku mvutano ukiendelea na kukiwa na hofu ya kuongezeka tena kwa mgogoro. Hata hivyo, Trump hakutoa ufafanuzi iwapo mazungumzo yataendelea au kama uwezekano wa hatua za kijeshi bado unazingatiwa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *