Serikali ya Kenya imetoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, pamoja na wananchi wa Tanzania kwa mapokezi ya kipekee na ukarimu waliouonyesha wakati wa Ziara ya Kihistoria ya Kitaifa iliyofanyika nchini humo.

Kupitia taarifa rasmi, Serikali ya Kenya imesisitiza dhamira yake ya kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa makubaliano mbalimbali yaliyosainiwa wakati wa ziara hiyo, ambayo yanalenga kuimarisha maendeleo ya pamoja na kukuza ustawi wa mataifa hayo mawili.

Serikali hiyo pia imeeleza kuwa itaendelea kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na ushirikiano wa pande mbili kati ya Kenya na Tanzania, sambamba na kuendeleza ushirikiano ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwa lengo la kuongeza muunganiko wa kikanda na ustawi wa pamoja.

Ziara hiyo ya Kitaifa ya siku mbili ilihitimishwa kwa hafla ya kuagana rasmi na Rais Samia Suluhu Hassan katika Ikulu ya Dodoma, baada ya majadiliano yenye mafanikio kati ya viongozi wa nchi hizo mbili.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *