Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA), Gianni Infantino, amethibitisha kupokea simu kutoka kwa Rais wa Marekani, Donald Trump, aliyehoji kuhusu adhabu ya kufungiwa kwa mshambuliaji wa timu ya taifa ya Marekani, Folarin Balogun. Infantino amebainisha kuwa alimweleza Trump kuwa suala hilo lipo mikononi mwa vyombo huru vya nidhamu vya FIFA ambavyo haziwezi kuingiliwa na uongozi wake.
Akizungumzia maamuzi yanayotolewa na Kamati ya Nidhamu ya shirikisho hilo, Infantino alikiri kuwa wakati mwingine hukumbana na mshangao.
“Wakati mwingine nakubaliana nayo (maamuzi ya kamati), na wakati mwingine sikubaliani nayo,” alisema Infantino, akisisitiza uhuru wa kamati hiyo.
Kufuatia msimamo huo, hatima ya Balogun inasalia mikononi mwa Kamati huru ya Nidhamu ya FIFA ambayo inatarajiwa kutoa uamuzi wa mwisho baada ya kukamilisha mapitio ya kesi yake.