Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema kuwa alipokea ujumbe kutoka kwa Kiongozi Mkuu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wiki iliyopita.Putin pia alimtakia Kiongozi Mkuu wa Iran afya njema na mafanikio, akisisitiza kuwa anatumai salamu zake za dhati zitawasilishwa kwake.Aidha, rais huyo wa Urusi alieleza kuwa nchi yake iko tayari kufanya juhudi zozote zitakazolinda maslahi ya Iran pamoja na nchi nyingine za eneo hilo, kwa lengo la kusaidia kurejesha amani katika Mashariki ya Kati kwa haraka iwezekanavyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *