Israel imepokea rasmi balozi wa kwanza kabisa wa Somaliland, Mohamed Hagi, ikiwa ni hatua muhimu ya kidiplomasia huku pande zote zikiahidi kuimarisha ushirikiano katika biashara, usalama na mahusiano ya kikanda.Balozi wa kwanza wa Somaliland kwenda nchi ya kigeni amewasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais wa Israel, Isaac Herzog, kufuatia utambuzi wa Israel wa uhuru wa eneo hilo lililojitenga mwaka jana.Somaliland ilitangaza kujitenga na Somalia mwaka 1991 lakini imeendelea kutotambuliwa kimataifa kwa zaidi ya miongo mitatu.