Makomando wa Israel leo wamevamia na kuzuia meli za msafara wa Global Sumud Flotilla (GSF) takribani maili 250 za baharini kutoka Gaza katika maji ya kimataifa. Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, amesema operesheni hiyo ilikuwa hatua ya kuzuia jaribio la kuvunja mzingiro wa Israel dhidi ya kundi la Hamas.

Taarifa zinaeleza kuwa mwezi uliopita vikosi vya Israel pia vilizuia boti 22 kutoka msafara huohuo karibu na kisiwa cha Krete. Katika tukio hilo, wanaharakati 181 walikamatwa kabla ya kuachiliwa baadaye kufuatia shinikizo na ukosoaji kutoka kwa jumuiya ya kimataifa.

Miongoni mwa waliokamatwa katika tukio la leo ni Dkt. Margaret Connolly, dada wa Rais wa Ireland, Catherine Connolly. Akizungumza jijini London baada ya mkutano na Mfalme Charles wa Uingereza, Rais Connolly amesema anajivunia ujasiri wa dada yake lakini pia ana wasiwasi kuhusu usalama wake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *