Kituo cha televisheni cha Channel 13 nchini Israel kimeripoti kuhusu mabadiliko ya mbinu za kivita za kundi la Hzb. Allah, kufuatia shambulio la hivi karibuni lililojeruhi wanajeshi wanne wa Israel.

aKwa mujibu wa taarifa hiyo, Hzb. Allah ilifanikiwa kutega kifaa cha mlipuko baada ya kufuatilia kwa karibu nyendo za vikosi vya Israel na kisha kukilipua. Kituo hicho kimeeleza kuwa kundi hilo sasa limerejea katika mbinu za vita vya msituni (guerrilla warfare).

Mbinu hii, ambayo haihitaji idadi kubwa ya wapiganaji, imetajwa kuwa na ufanisi mkubwa uwanjani kwa kuvifuatilia, kuvichosha, na kuvisababishia hasara vikosi vya Israel.

Katika uchambuzi wake, Channel 13 imefananisha hali inayoendelea hivi sasa na ile ya miaka ya 1990 katika eneo lililojulikana kama “ukanda wa usalama” kusini mwa Lebanon, ikibainisha kuwa mazingira ya sasa yanaakisi kikamilifu hali halisi ya kipindi hicho.

Kutokana na hali hiyo uwanjani, kituo hicho kimehitimisha kwa kusema kuwa, kufikiwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano kikamilifu na mara moja utakuwa ni “uamuzi sahihi” hasa endapo utatangazwa sasa na Rais wa Marekani, Donald Trump.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *