Washington, Marekani — Vyanzo vya shirika la habari la CBS vimeripoti kuwa meli za kivita za Marekani, USS Truxtun na USS Mason, zimeshambuliwa vikali na vikosi vya Iran katika Bahari ya Oman.
Maafisa wa Marekani wameeleza kuwa mashambulizi hayo yalikuwa makubwa na ya muda mrefu zaidi ikilinganishwa na yale yaliyotekea siku kadhaa zilizopita.Kwa mujibu wa taarifa hiyo, boti za kasi za Iran zilikaribia manowari hizo kwa umbali hatari, hali iliyozilazimisha meli za Marekani kutumia mizinga ya baharini, mfumo wa silaha za kujihami za karibu (CIWS) pamoja na bunduki zilizowekwa juu ya staha.
AAidha, maafisa wa Marekani wamesema kuwa Iran ilitumia ndege zisizo na rubani (drones) na makombora katika oparesheni hiyo, jambo lililoonyesha ongezeko la uhasama na hatari katika eneo la ghuba.