Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Urusi, Dmitry Medvedev, amesema kuwa mvutano unaoendelea kati ya Marekani na nchi za Ulaya unaweza hatimaye kupelekea ushindi kwa Urusi.
Akizungumza kuhusu hali ya kisiasa ya kimataifa, Medvedev alieleza kuwa ni “jambo la kufurahisha” kutazama jinsi mahusiano kati ya Marekani na Ulaya yanavyozorota siku hadi siku.Wachambuzi wa kisiasa wanaona kauli hiyo kama ishara ya kujiamini kwa Urusi katika mazingira ambamo uhusiano wa Marekani na mataifa mengine duniani unaonekana kuzorota.