WASHINGTON – Mpango wa amani wa Rais Trump nchini Gaza unaonekana kulegalega kufuatia uamuzi wa Marekani wa kufunga kituo chake kikuu cha uratibu wa kijeshi (CMCC).

Hatua hii inajiri huku kukiwa na ukosoaji mkubwa kwamba kituo hicho kimeshindwa kusimamia makubaliano ya kusitisha mapigano au kuboresha hali ya utoaji wa misaada ya kibinadamu katika eneo hilo.Inaripotiwa kuwa shughuli za kituo hicho sasa zitahamishiwa chini ya usimamizi wa kikosi kipya cha kimataifa, ambacho kitakuwa na idadi ndogo ya wanajeshi wa Marekani ikilinganishwa na hapo awali.

Hata hivyo, wachambuzi wa mambo wanasema kuwa mustakabali wa mpango huo mzima bado ni wa mashaka. Hii inatokana na kuendelea kwa mashambulizi kutoka kwa jeshi la Israel huku kundi la Hamas likionekana bado limeimarika katika ngome zake, jambo linalofanya juhudi za kuleta utulivu kukwama na kukubaki kwenye hali ya sintofahamu.

Chanzo: Reuters

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *