Hossein Vafaei wa Iran amepata ushindi muhimu baada ya kumshinda Judd Trump, anayeshika nafasi ya kwanza duniani katika mchezo wa snuka. Katika pambano lililodumu kwa raundi tatu, Vafaei alifanikiwa kumtungua Trump na kufuzu kuingia katika hatua ya wachezaji nane bora duniani. Ushindi huo unaimarisha nafasi ya Vafaei katika mashindano hayo na kuvutia macho ya wapenzi wa snuka duniani.Baada ya ushindi huo Hossein Vafaei ameingia miongoni mwa wachezaji 8 bora duniani.