Marabi wakuu wa Kiyahudi wa mrengo wa maendeleo nchini Uingereza wameonya kuwa mwelekeo wa sasa wa kisiasa wa Israel unawakilisha tishio kubwa kwa maadili na utambulisho wa Kiyahudi, wakisisitiza kuwa ukosoaji wa serikali ya Israel ni “wajibu wa Kiyahudi,” si kitendo cha kukosa uaminifu.Rabbi Charley Baginsky na Rabbi Josh Levy, wanaoongoza Uyahudi wa Maendeleo unaowakilisha takriban theluthi moja ya masinagogi nchini Uingereza, walisema kuwa mwelekeo wa Israel unaweza kuwa “hauendani na maadili ya Kiyahudi” na unaweza kuleta “tishio la kuwepo” kwa Uyahudi wenyewe.Levy alisema kuwa kujihusisha na sera za Israel ni sehemu ya “mazungumzo ya Kiyahudi ya milenia” kuhusu maadili na uwajibikaji, akidai kuwa Wayahudi hawawezi kutenganisha utambulisho wao wa kidini na matendo ya dola ya Israel.Baginsky aliongeza kuwa Uzayuni wa kidini lazima ujumuishe kutambua haki ya Wapalestina kujitawala, akipinga tafsiri za mrengo mkali wa kulia za Uzayuni zinazokuzwa na wanasiasa wa Israel.