BERLIN, UJERUMANI – Serikali ya Ujerumani imepinga vikali wito wa rais mteule wa Marekani, Donald Trump, wa kuitaka nchi hiyo kutoa ahadi ya utiifu usio na masharti kwa shirika la kijeshi la NATO.

Katika kile kinachotafsiriwa kama msimamo thabiti dhidi ya shinikizo la Washington, Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani, Boris Pistorius, amesisitiza kuwa NATO si jukwaa la kufuata amri za upande mmoja.

Akizungumza na waandishi wa habari kufuatia ripoti hiyo ya gazeti la Der Spiegel, Pistorius alibainisha kuwa ushirikiano wa kijeshi wa NATO umejengwa juu ya msingi wa makubaliano ya pamoja na si utiifu wa kipofu.

“NATO si shirika la kufuata amri bila kutafakari. Maamuzi yote ya muungano huu hufanywa kupitia makubaliano huru ya nchi zote wanachama, na si kwa kudhibitiwa au kulazimishwa na nchi yoyote moja,” alisema Pistorius.

Kauli hii inakuja wakati ambapo kumeibuka wasiwasi wa kidiplomasia kuhusu mustakabali wa ushirikiano wa kiusalama kati ya Marekani na washirika wake wa Ulaya chini ya utawala ujao wa Trump.

Leave a Reply