Akiba ya kimkakati ya mafuta nchini Marekani imeripotiwa kupungua kwa kiasi kikubwa na kufikia kiwango cha chini zaidi kuwahi kushuhudiwa katika kipindi cha miaka 43 iliyopita.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari za Nishati nchini Marekani (EIA), makampuni ya nishati ya nchi hiyo yalitoa jumla ya mapipa milioni 5.5 ya mafuta ghafi kutoka kwenye bohari kuu la Akiba ya Kimkakati ya Mafuta (SPR) katika wiki iliyoishia tarehe 26 Juni.

Kutokana na hatua hiyo, akiba ya mafuta ya dharura ya nchi hiyo sasa imeshuka hadi kufikia mapipa milioni 325.7, kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa tangu mwezi Mei mwaka 1983.

Kupungua huku kwa akiba kunaashiria shinikizo kubwa katika soko la nishati la Marekani wakati huu kukiwa na mahitaji makubwa ya mafuta.

Leave a Reply