Serikali ya Ufaransa imethibitisha kisa chake cha kwanza cha ugonjwa wa Ebola kinachohusiana na mripuko unaoendelea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Kisa hicho kimebainika baada ya daktari mmoja, aliyekuwa akirejea nchini humo akitokea katika misheni ya kutoa misaada ya kibinadamu, kupimwa na kukutwa na virusi vya ugonjwa huo.

Mgonjwa huyo tayari amewekwa chini ya uangalizi maalum na ametengwa (isolation) ili kuzuia maambukizi zaidi. Wakati huo huo, mamlaka za afya nchini Ufaransa zimeanza mchakato wa kuwatafuta na kuwafuatilia watu wote waliokuwa karibu au kugusana na daktari huyo (contact tracing).

Pamoja na kutokea kwa kisa hicho, maafisa wa afya wametoa wito wa utulivu, wakieleza kuwa hatari ya kusambaa kwa ugonjwa huo kwa idadi kubwa ya watu barani Ulaya bado ni ndogo sana kutokana na mifumo imara ya afya iliyopo.

Leave a Reply