BEIRUT, LEBANON – Hali ya usalama nchini Lebanon imeendelea kuwa tete baada ya jeshi vamizi la Israel (IOF) kutangaza leo Ijumaa kuwa wanajeshi wake wanne wameuawa usiku wa kuamkia leo kufuatia shambulio lililotekelezwa na kundi la h3zb0//ah kusini mwa nchi hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa ya jesh hilo, shambulio hilo lilitokea katika kijiji cha Kfar Tebnit. Saa chache baada ya vifo hivyo, wanajeshi wengine watano wa Israel walijeruhiwa vibaya katika eneo hilo hilo, huku operesheni za kijeshi zikishika kasi.

Maafa Upande wa Lebanon
Wakati mapigano yakizidi kupamba moto, Wizara ya Afya nchini Lebanon imeripoti kuwa takriban watu 18 wameuawa kufuatia mfululizo wa mashambulizi ya anga yaliyofanywa na ndege za kivita za Israel.

Kuvunjika kwa Makubaliano ya Amani?
Ongezeko hili la ghasia linakuja wakati ambapo ulimwengu ulikuwa na matumaini ya kusitishwa kwa mapigano. Mapema wiki hii, Marekani na Iran zilifikia maelewano (MoU) iliyozitaka nchi hizo na washirika wao kusitisha uhasama nchini Lebanon mara moja.

Licha ya juhudi hizo za kidiplomasia, hali halisi uwanjani inaonyesha kuwa pande zote mbili bado zinatunishiana misuli. Israel imeendelea kufanya mashambulizi makali ya anga huku H3zb0//ah, kundi linaloungwa mkono na Iran, likijibu kwa mashambulizi dhidi vikosi vya Israel vinavyokalia Lebanon kimabavu, jambo linalotishia kuvunjika kwa makubaliano hayo ya amani kabla hata hayajaanza kutekelezwa kikamilifu.

Hadi sasa, mataifa ya kigeni yanaendelea kutoa wito wa utulivu huku hofu ikitanda kuwa mzozo huo unaweza kusambaa na kuwa vita kubwa zaidi ya kikanda.

Leave a Reply