Rais wa Marekani, Donald Trump, amezua mjadala mzito katika mkutano wa kilele wa G7 nchini Ufaransa baada ya kuishauri Israel “kuiachia Syria ishughulikie kundi la Hezbollah.” Trump amedai kuwa Syria ingefanya kazi nzuri zaidi katika kukabiliana na kundi hilo kuliko upande mwingine wowote.
Kauli hii ya Trump inakuja ikiwa ni mwendelezo wa mahojiano yake na kituo cha NBC wiki iliyopita, ambapo alitaka kuwepo kwa operesheni maalum na ya haraka dhidi ya Hezbollah (inayofadhiliwa na Iran), huku akisisitiza kuwa Syria inapaswa kuhusika kikamilifu.
Hata hivyo, pendekezo hilo linaonekana kukumbwa na changamoto za kidiplomasia. Ingawa serikali mpya ya Syria chini ya Rais Ahmed al-Sharaa imeanza kudhibiti mitandao ya ulanguzi ya Hezbollah ndani ya mipaka yake, haijaonyesha nia yoyote ya kuingia kijeshi nchini Lebanon.
Wataalamu wa mambo wanasema hatua yoyote ya Syria kuvuka mpaka inaweza kuibua “bomu la kisiasa,” kwani itapingwa vikali na serikali ya Lebanon na kuamsha kumbukumbu chungu za uvamizi wa Syria nchini humo uliodumu kwa takriban miaka 30