Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Leo XIV, ametoa kauli ya shukrani akisema “Mungu ashukuriwe” baada ya mataifa ya Marekani na Iran kutangaza rasmi kusitisha mapigano na kuanza mpango wa kusaka amani ya kudumu katika ukanda wa Mashariki ya Kati.

Papa Leo XIV, ambaye ni Papa wa kwanza katika historia kutokea nchini Marekani, amekuwa na msimamo mkali dhidi ya vita hivyo, hali iliyopelekea huko nyuma kurushiana maneno na Rais Trump. Hata hivyo, akizungumza na waandishi wa habari nje ya makazi yake huko Castel Gandolfo, nchini Italia, Papa ameeleza matumaini yake kuwa makubaliano hayo yatakuwa mwisho wa mauti na uharibifu.

“Bado kuna mambo kadhaa ya kurekebisha, lakini ni bora zaidi kufanya hivyo kupitia mazungumzo na majadiliano badala ya kurejea vitani,” alisema Papa Leo. Amesisitiza kuwa anaomba suluhu hiyo iwe ya kweli ili ulimwengu uweze kusonga mbele kwa amani.

Leave a Reply