NEW DELHI, INDIA– Wizara ya Mambo ya Nje ya India imewasilisha malalamiko rasmi kwa mwanadiplomasia wa Marekani, ikielezea kutoridhishwa kwake na vitendo vya majeshi ya wanamaji ya Marekani dhidi ya meli za kibiashara.

Onyo hilo limekuja baada ya jeshi la Marekani kushambulia meli mbili za India na kuuwa mabaharia watatu wananchi wa India.

Katika tamko hilo kali, Serikali ya India imesisitiza kuwa shambulizi lolote dhidi ya meli za kibiashara ni jambo lisilokubalika na haliwezi kuvumiliwa. India imeeleza kuwa hatua hizo za kijeshi zinaashiria tishio la moja kwa moja kwa usalama na utulivu wa biashara ya kimataifa ya baharini.

Wizara hiyo imebainisha kuwa matendo hayo yanakuja katika kipindi ambacho dunia inapitia wakati mgumu na katika eneo ambalo ni muhimu kiuchumi na kimkakati kwa usafirishaji wa bidhaa duniani.

India imetaka hatua za haraka zichukuliwe ili kulinda usalama wa njia za bahari na kuepuka kuzorota zaidi kwa hali ya usalama wa kimataifa, ikisisitiza kuwa utulivu wa bahari ni nguzo muhimu kwa ustawi wa uchumi wa mataifa mengi duniani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *