BANDAR ABBAS, IRAN — Chanzo cha kuaminika cha kijeshi kimeiambia Wakala wa Habari wa Tasnim kuwa, usiku wa kuamkia Alhamisi, meli moja ya mafuta ya Marekani ilijaribu kupita kwa siri katika Mlango wa Hormuz baada ya kuzima mifumo yake ya rada.

Hata hivyo, kufuatia hatua ya haraka na madhubuti ya Kikosi cha Wanamaji cha Walinda Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC), ikiwemo kufyatua risasi za tahadhari kuelekea meli hiyo, chombo hicho kililazimika kusitisha safari yake na kurejea kilikotoka.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, katika kujibu tukio hilo, jeshi la Marekani lilifyatua mashambulizi kuelekea eneo la ardhi tupu lililoko karibu na Bandar Abbas. Sauti za milipuko zilizosikika katika maeneo ya karibu zinaripotiwa kuhusishwa na tukio hilo.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa mashambulizi hayo hayakusababisha vifo, majeruhi wala uharibifu wa mali.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *