Mfumuko wa bei ya mafuta nchini Marekani umeingia katika hatua mpya, huku ukizidi kutishia uchumi wa wananchi wake.

Kampuni kubwa ya rejareja nchini humo, Walmart, imetoa onyo ikieleza kuwa kupanda kwa bei ya nishati hiyo, kufuatia mgogoro wa Mlango wa Bahari wa Hormuz, kumeongeza msukumo na mzigo mzito wa kimaisha kwa kaya nyingi za Wamarekani.

Kwa mujibu wa takwimu, bei ya galoni moja ya mafuta nchini Marekani imepaa kutoka takriban dola $3 hadi dola $4.56. Kufuatia hali hii, kampuni ya Walmart imetabiri kuwa ukuaji wa mauzo yake utashuka katika miezi ijayo.

Aidha, wakurugenzi wa kampuni hiyo wametoa tahadhari kuwa endapo mgogoro huo utaendelea, unaweza kusababisha kupanda zaidi kwa bei za vyakula na hatimaye kupunguza uwezo wa manunuzi kwa walaji nchini Marekani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *