Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi, amewahimiza wananchi kupunguza matumizi ya petroli na dizeli kwa kuhamasisha matumizi ya usafiri wa umma na njia mbadala za nishati.

Katika wito wake, Modi alisema kuwa wakazi wa miji yenye huduma za metro wanapaswa kuipa kipaumbele metro kama njia kuu ya usafiri. Pia aliwataka wananchi kutumia mfumo wa kushirikiana magari (carpool) wanapolazimika kusafiri kwa magari binafsi ili kupunguza matumizi ya mafuta.

Vilevile, alisisitiza umuhimu wa kutumia reli za umeme kusafirisha bidhaa, akieleza kuwa njia hiyo husaidia kupunguza matumizi ya petroli na dizeli. Aidha, aliwahimiza watu wenye magari ya umeme kuyatumia mara kwa mara ili kuchangia juhudi za kupunguza utegemezi wa mafuta.

Modi pia alikumbusha kuwa wakati wa janga la Corona, India iliimarisha matumizi ya mikutano ya video, mikutano ya mtandaoni na mfumo wa kufanya kazi kutoka nyumbani. Alisema mifumo hiyo inapaswa kuendelea kutumika kwa kuwa ina manufaa kwa nchi.

Aliongeza kuwa kazi kutoka nyumbani, mikutano ya mtandaoni na vikao vya kidijitali vinapaswa kupewa kipaumbele kama sehemu ya juhudi za kupunguza matumizi ya nishati na kuongeza ufanisi katika kazi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *