Wakatoliki nchini Lebanon wameeleza masikitiko yao kufuatia picha iliyoenea mtandaoni ikimuonyesha askari wa Israeli akivuta sigara akiwa ameishirikisha sanamu ya Bikira Maria.

Tukio hilo liliripotiwa kutokea katika kijiji cha Kikristo cha Debel, kusini mwa Lebanon.Kwa mujibu wa vyanzo vya eneo hilo, kijiji cha Debel ndicho hicho hicho ambako mwezi uliopita askari wa Israeli alihusishwa na kitendo cha kuvunja sanamu ya Yesu Kristo.

Matukio hayo yamezua hofu na malalamiko miongoni mwa jumuiya za Kikristo nchini Lebanon, ambazo zinadai visa vya askari wa Israeli kudhihirisha kutoheshimu imani yao vinaendelea kuongezeka.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *