Jeshi la Israel limezuia msafara wa Global Sumud Flotilla katika maji ya kimataifa, na kukamata meli 21, kulingana na waandaaji wa msafara huo.Takribani wanaharakati 175, wakiwemo raia wa Uturuki, walikamatwa, huku meli 17 zikiwa zimefanikiwa kufika kwenye maji ya Ugiriki.

Msafara huo, uliokuwa umebeba zaidi ya raia 400, ulikuwa na lengo la kupeleka misaada ya kibinadamu katika eneo la Ukanda wa Gaza lililozingirwa.Uturuki imelaani operesheni hiyo ikiitaja kama “kitendo cha uharamia”, ikishutumu Israel kwa kukiuka sheria za kimataifa na kulenga msafara wa kibinadamu uliokuwa na lengo la kuangazia kuzorota kwa hali ya kibinadamu Gaza.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *