Rais wa Marekani, Donald Trump, ameripotiwa kumtaka Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, kutotoa jibu la haraka kufuatia shambulio la makombora, na badala yake kusubiri kwa siku chache ili kutoa nafasi kwa juhudi za kidiplomasia kuendelea.
Kwa mujibu wa Channel 12 ya Israel, Trump alimweleza Netanyahu kutoingilia mchakato wa mazungumzo unaoendelea. Afisa mmoja mwandamizi wa Marekani amesema Netanyahu awali alipinga ombi hilo, lakini baadaye alikubali kwa kiasi kusitisha hatua za kujibu shambulio hilo wakati mazungumzo yakiendelea.
Taarifa hiyo inakuja huku juhudi za kidiplomasia zikiendelea kutafuta suluhu ya mvutano unaohusisha Israel na Iran.