TEHRAN – Ripoti mpya ya shirika la habari la Bloomberg imebainisha kuwa, tangu kuanza kwa mzozo wa sasa, Iran imefanikiwa kutungua zaidi ya ndege zisizo na rubani (drones) za Marekani aina ya MQ-9 Reaper, idadi ambayo ni zaidi ya 24.Hatua hiyo imesababisha pigo kubwa kwa jeshi la Marekani, huku ikikadiriwa kusababisha hasara ya kifedha inayokaribia dola bilioni 1. Takwimu hizo zinaonesha kuwa uharibifu huo umepunguza kwa takriban 20% uwezo wa jeshi la Marekani (Pentagon) katika kundi la ndege hizo walizokuwa nazo kabla ya kuanza kwa mzozo huu.Uchambuzi wa wataalamu wa kijeshi unaonesha kuwa kupotea kwa ndege hizi za kisasa za upelelezi na mashambulizi ni changamoto kubwa kwa mkakati wa anga wa Marekani katika ukanda huu.