BRUSSELS/TEHRAN – Umoja wa Ulaya (EU) leo umetangaza uamuzi wa kupanua mfumo wake wa vikwazo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Hatua hii imetajwa na upande wa Iran kama kitendo dhidi ya taifa hilo, ambacho kinapuuza haki yake ya kisheria ya kusimamia usalama wa usafiri wa majini katika Mlango wa Bahari wa Hormuz, ambao sehemu yake ipo ndani ya mamlaka ya maji ya Iran.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, vikwazo hivi vipya vitawalenga watu binafsi na taasisi mbalimbali.
WUmoja wa Ulaya unadai kuwa walengwa wa vikwazo hivi ni wale wanaohusika na vitendo vinavyolenga kutishia uhuru na usalama wa usafiri wa baharini katika ukanda wa Asia Magharibi, hususan katika eneo la kimkakati la Mlango wa Bahari wa Hormuz.