Kulingana na duru za kijeshi kutoka nchini Israeli zilizokaririwa na shirika la habari la Kan News, majeshi ya Marekani na Israeli yamewekwa katika hali ya tahadhari ya juu, yakijiandaa kwa uwezekano wa kuanzisha tena mashambulizi dhidi ya Iran.

Imeelezwa kuwa operesheni yoyote mpya ya kijeshi itakayofanyika itakuwa ni ya ushirikiano wa pamoja kati ya mataifa hayo mawili.Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mikakati ya sasa ya Israeli inalenga hasa kushambulia na kudhoofisha miundombinu mikuu ya nishati ya taifa la Iran.

Serikali ya Israeli inaamini kuwa hatua hii itaishinikiza Tehran kulegeza msimamo wake katika meza ya mazungumzo. Hata hivyo, wachambuzi wa masuala ya kiusalama wanaonyesha wasiwasi wao, wakitilia shaka ikiwa shinikizo hilo la kijeshi litaifanya Iran kusalimu amri na kukubaliana na matakwa hayo.

Katika hatua inayoashiria uzito wa hali hiyo, imeripotiwa kuwa Donald Trump na Waziri Mkuu wa Israeli, Benjamin Netanyahu, wamefanya mazungumzo ya simu ya zaidi ya dakika 30 hii leo. Katika mazungumzo hayo, suala la uwezekano wa kurejea katika mapigano lilijadiliwa kwa kina. Maafisa wa ngazi za juu wa Israeli wameweka wazi na kusisitiza kuwa, hatima na uamuzi wa mwisho wa kuanzisha tena mapigano hayo upo mikononi mwa Donald Trump.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *