Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC) yenye makao yake The Hague imetangaza kuwa mshukiwa wa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 nchini Rwanda, Félicien Kabuga, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 90.
Taarifa zinaeleza kuwa Kabuga alifariki Jumamosi alipokuwa akipatiwa matibabu hospitalini, huku Jaji Graciela Gatti Santana ameamuru uchunguzi wa haraka kufanyika ili kubaini chanzo cha kifo hicho.Kabuga alikuwa miongoni mwa watu waliotafutwa zaidi duniani kwa tuhuma za kuhusika katika kupanga na kuchochea mauaji ya takribani watu laki nane waliouawa kati ya Aprili na Juni 1994 nchini Rwanda.
Alikamatwa nchini Ufaransa mwaka 2020 kabla ya kuhamishiwa The Hague, ambako alikabiliwa na mashtaka ya mauaji ya kimbari, njama za kutekeleza mauaji hayo pamoja na uhalifu dhidi ya ubinadamu.