Ufaransa imeanzisha rasmi uchunguzi wa kisheria kuhusu mauaji ya mwaka 2018 ya mwanahabari Jamal Khashoggi, uchunguzi unaomlenga Mwanamfalme wa Saudi Arabia, Mohammed bin Salman.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, jaji kutoka kitengo cha uhalifu dhidi ya ubinadamu nchini Ufaransa ameteuliwa kusimamia uchunguzi huo.
Hii ni mara ya kwanza kwa jaji wa Ufaransa kuteuliwa rasmi kuchunguza madai yanayohusisha nafasi inayodaiwa ya Mohammed bin Salman katika tukio hilo.Hadi sasa, Saudi Arabia haijatoa tamko lolote kuhusu maendeleo hayo.