BEIJING: Katika kile kinachoonekana kama hatua kali za kiusalama, wajumbe wa Marekani wameripotiwa kutupa zawadi zote walizopewa na wenyeji wao nchini China kabla ya kupanda ndege ya Rais, Air Force One.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mwandishi wa gazeti la New York Post, wajumbe hao walionekana wakitupa nishani, pini na vitu mbalimbali vya ukumbusho kwenye mapipa ya taka uwanjani hapo kabla ya kuanza safari ya kuondoka jijini Beijing.

Ripoti hiyo inafafanua zaidi kuwa, uamuzi huo ulitokana na agizo maalum la kutoruhusu kifaa chochote chenye asili ya China kuingizwa ndani ya ndege hiyo kwa hofu ya udukuzi.

Katika kuimarisha usalama huo wa kimtandao, wajumbe hao hawakuruhusiwa kusafiri na simu zao binafsi wakati wa ziara hiyo. Badala yake, walipatiwa simu maalum zilizokuwa zimesafishwa taarifa zote na ambazo zilidhibitiwa kiusalama.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *