Rais wa Marekani Donald Trump ametoa matamshi makali kuhusu Iran na vyombo vya habari vya Marekani, akidai kuwa baadhi ya taarifa zinazotolewa kuhusu uwezo wa kijeshi wa Iran ni za uongo na zinachangia kuipa Iran matumaini yasiyo ya kweli.

Katika kauli yake, Trump alisema kuwa vyombo vya habari vinavyoonyesha Iran kuwa inaendelea vizuri kijeshi dhidi ya Marekani vinafanya jambo linalokaribia usaliti. Pia aliwashutumu baadhi ya Wamarekani kwa kutokuwa waaminifu kwa nchi yao.

Trump alidai kuwa jeshi la majini la Iran limeharibiwa kabisa, huku akisema kuwa meli zote za kijeshi za Iran zimezama. Aidha, alisema kuwa jeshi la anga la Iran pamoja na teknolojia yake ya kijeshi vimeangamizwa, na kwamba viongozi wa nchi hiyo hawapo tena madarakani.

Aliongeza kuwa uchumi wa Iran uko katika hali mbaya.Mwisho wa taarifa yake, Trump alisema kuwa ni watu “washindwa, wasio na shukrani na wapumbavu” pekee wanaoweza kuipinga Marekani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *