Shirika la habari la Reuters limeripoti kuwa Saudi Arabia ilifanya mashambulizi kadhaa ya anga dhidi ya Iran mwishoni mwa mwezi Machi, ikiwa ni hatua ya kujibu mashambulizi ya makombora na ndege zisizo na rubani (droni) yaliyolenga Ufalme huo.

Kwa mujibu wa maafisa wa Magharibi na Iran walionukuliwa na Reuters, mashambulizi hayo yalitekelezwa na Jeshi la Anga la Saudi Arabia kama hatua ya kulipiza kisasi baada ya Saudi Arabia kushambuliwa. Hata hivyo, maeneo yaliyolengwa ndani ya Iran bado hayajawekwa wazi.

Ripoti hiyo inaeleza kuwa Saudi Arabia iliijulisha Iran mapema kabla ya kutekeleza mashambulizi hayo. Baadaye, pande hizo mbili zilifanya mawasiliano ya kina ya kidiplomasia huku Riyadh ikitoa onyo kuhusu uwezekano wa hatua nyingine za kijeshi iwapo mashambulizi dhidi yake yangeendelea.

Hatimaye, mawasiliano hayo yalisaidia kufikiwa kwa makubaliano ya kupunguza mvutano kati ya nchi hizo mbili na kuendeleza juhudi za kutuliza hali ya mzozo katika eneo hilo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *