Marekani Yatangaza Kuwasili kwa Manowari ya Nyuklia Gibraltar.
Jeshi la Wanamaji la Marekani limethibitisha hadharani kuwasili kwa manowari ya makombora ya balistiki ya daraja la Ohio katika eneo la Gibraltar, katika hatua nadra inayochukuliwa kama ishara ya kuonyesha nguvu.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, uamuzi wa kutangaza hadharani harakati za manowari hiyo umevutia hisia za wachambuzi wa masuala ya usalama, kwani kwa kawaida vyombo hivyo hutumwa kwa usiri mkubwa kutokana na nafasi yake ya kimkakati katika mfumo wa silaha za nyuklia.
Tangazo hilo linakuja wakati mvutano ukiendelea kuhusiana na mazungumzo ya kimataifa, usalama wa Mlango wa Hormuz, pamoja na kuongezeka kwa taharuki kati ya Marekani, Israel na Iran.
Wataalamu wanasema hatua hiyo inaweza kutafsiriwa kama ujumbe wa kisiasa na kijeshi unaolenga kuashiria msimamo wa Marekani katika eneo hilo.