Waziri Mkuu wa zamani wa Qatar, Hamad bin Jassim Al Thani, amesema kuwa Iran imekuwa na nguvu zaidi kisiasa kufuatia mashambulizi yaliyofanywa na Marekani pamoja na Israel.
Alieleza kuwa juhudi zozote za kujaribu kuipindua Iran kwa kutumia nguvu za kijeshi zilikuwa hazina uwezekano wa kufanikiwa tangu mwanzo.
Aidha, Al Thani alisema kuwa Iran inaweza kutumia uzoefu wa vita kuimarisha uwezo wake wa kijeshi na maendeleo ya teknolojia, akiongeza kuwa nchi za Ghuba pia zinapaswa kufanya hivyo ili kuongeza uwezo wao wa kujilinda.