Meli ya kubeba gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG) inayomilikiwa na Qatar, iitwayo “Al‑Khariyat”, imetuma ishara katika maji ya Bahari ya Oman, kulingana na taarifa za ufuatiliaji wa meli.
Taarifa zinaonyesha kuwa meli hiyo ilionekana jana katika eneo la lango la Mlango wa Hormuz kabla ya kuzima mfumo wake wa utambuzi wa kiotomatiki wa meli (AIS).Meli hiyo inaripotiwa kuelekea Pakistan.
Vyanzo vinaeleza kuwa huenda ikawa meli ya kwanza isiyohusiana na Iran kuruhusiwa kupita katika Mlango wa Hormuz na Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu tangu kuanza kwa kile kinachotajwa kama mzingiro au vitendo vya uharamia wa baharini vinavyohusishwa na Marekani.