Mwakilishi wa Chama cha Democratic katika Bunge la Marekani, Seth Moulton, amesema kuwa rais wa Marekani Donald Trump ni tishio kwa usalama na uthabiti wa Marekani.

Akizungumza kuhusu wasiwasi unaoibuka juu ya umri na mwenendo wa Trump, Moulton alisema ni kawaida kwa watu wanapozeeka kupungua uwezo wao wa kufanya maamuzi, lakini hali hiyo inaweza kuwa hatari zaidi inapomhusu mtu anayewania au kushika nafasi muhimu ya uongozi wa taifa.

Moulton alisisitiza kuwa, kwa maoni yake, wananchi wengi wanaona Trump kuwa hatari kwa wanajeshi wa Marekani, uchumi wa nchi pamoja na usalama wa taifa.

wAliongeza kuwa orodha ya masuala yanayozua wasiwasi kuhusu Trump ni ndefu, akisema pia kwamba kwa sasa Trump anaonekana kuwa hatari zaidi kuliko alivyokuwa wakati wa muhula wake wa kwanza wa urais.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *