WASHINGTON, DC - MAY 22: Sen. JD Vance (R-OH) gestures while speaking during a news conference on Capitol Hill on May 22, 2024 in Washington, DC. Senate Democrats have revived the bipartisan border bill that was already blocked once earlier this year, and Republicans including Sen. James Lankford (R-OK), who negotiated the immigration package say they will block it again. (Photo by Kent Nishimura/Getty Images)

WASHINGTON, Julai 16 – Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, amedai kuwa Israel inafadhili baadhi ya washawishi wa mitandao ya kijamii (social media influencers) ili kumshambulia kutokana na msimamo wake wa kuunga mkono mazungumzo na Iran pamoja na kuweka mbele juhudi za amani badala ya mivutano ya kijeshi.


Vance alitoa kauli hiyo akieleza kuwa mashambulizi dhidi yake mtandaoni yanahusishwa na msimamo wake kuhusu diplomasia na mazungumzo kati ya Marekani na Iran. Hata hivyo, hakuwasilisha ushahidi hadharani kuthibitisha madai hayo.


“Israel inalipa washawishi wa mitandao ya kijamii kunishambulia kwa sababu ninatetea mazungumzo na Iran na ninatanguliza amani,”

Vance alinukuliwa akisema.
Kauli hiyo imezua mjadala mpana kuhusu nafasi ya mitandao ya kijamii katika siasa za kimataifa na tofauti za mitazamo kuhusu sera ya Marekani kuelekea Mashariki ya Kati, hususan uhusiano wake na Israel na Iran.
#utaridi

Leave a Reply