Katika hali inayoweza kuibua mjadala mzito wa kisheria na kidiplomasia duniani, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya nchi za Magharibi (NATO) ameweka wazi ushiriki wa moja kwa moja wa mataifa ya Ulaya katika operesheni za kijeshi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

Katika ukiri uliopokelewa kwa mshtuko, kiongozi huyo wa NATO amethibitisha kuwa katika kipindi cha wiki kadhaa za mapigano, takriban ndege 5,000 za kivita za Marekani ziliruka kutoka kwenye vituo vya kijeshi vilivyoko barani Ulaya kuelekea nchini Iran kwa ajili ya kutekeleza mashambulizi.

Ushiriki wa Ulaya na Marekani

Kauli hiyo inabainisha kuwa nchi za Ulaya hazikuwa watazamaji tu, bali zilitoa miundombinu yao muhimu na maeneo ya kimkakati kuwezesha nguvu za anga za Marekani kupenya katika anga la Iran. Hii inatajwa kama ushirikiano wa kijeshi uliopangwa kwa kina kati ya Washington na washirika wake wa Ulaya.

Leave a Reply