Rais Donald Trump amezindua ndege mpya ya muda itakayotumiwa na rais katika Kituo cha Jeshi cha Andrews, huko Maryland.

Ndege hiyo ya kifahari, ambayo ni msaada kutoka nchi ya Qatar, imebadilishwa mwonekano wake kwa kupakwa rangi za bendera ya Marekani—nyekundu, nyeupe, na bluu—na kuandikwa maneno “United States of America” pembeni.

Kulingana na maelezo ya Ikulu ya Marekani, ndege hii itatumika kama hatua ya muda ya mpito. Hii ni kutokana na ukweli kwamba ndege mbili mpya za Air Force One zinazotengenezwa na kampuni ya Boeing bado hazijakamilika, huku zikikadiriwa kuchukua takriban miaka miwili zaidi kabla ya kuanza kazi rasmi.

Hii inafanya ndege hiyo mpya kutoka Qatar kuwa suluhisho la haraka ili kuhakikisha shughuli za usafiri wa kiongozi mkuu wa taifa zinaendelea bila kizuizi.

#utaridi

Leave a Reply