Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan na Rais wa Mpito wa Venezuela Delcy Rodríguez wamejadili namna ya kupanua ushirikiano kati ya nchi hizo katika sekta za biashara, nishati na uchimbaji madini.
Katika mazungumzo yao yaliyofanyika Jumatatu, viongozi hao walitathmini pia hatua mbalimbali zinazolenga kuongeza thamani ya biashara kati ya Uturuki na Venezuela kufikia dola za Marekani bilioni 3.
Aidha, Erdoğan na Rodríguez walibadilishana mawazo kuhusu maendeleo ya kikanda na ya kimataifa yanayoendelea kwa sasa.
Rais Erdoğan alithibitisha tena uungwaji mkono wa Uturuki kwa Venezuela na kusisitiza dhamira ya Ankara ya kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati ya mataifa hayo katika sekta mbalimbali.