Ukraine imefikia makubaliano na Sweden ya kupata jumla ya ndege 36 za kivita aina ya JAS 39 Gripen, katika hatua inayotarajiwa kuimarisha uwezo wa Jeshi la Anga la Ukraine. Kwa mujibu wa makubaliano hayo, Sweden itatoa ndege 16 za Gripen C/D kama msaada, huku ndege nyingine 20 za Gripen E/F zikiuzwa kwa Ukraine.

Taarifa zinaeleza kuwa ndege za Gripen C/D zinatarajiwa kuwasili mwaka 2027, wakati ndege za Gripen E/F zikipangwa kuwasili mwaka 2030.

Wachambuzi wa masuala ya ulinzi wanasema kuwa ndege za Gripen C/D zitakuwa nyongeza muhimu kwa Ukraine kutokana na uwezo wake wa kutumia njia fupi za kurukia ndege pamoja na kuhitaji muda mfupi wa matengenezo kabla ya kuanza tena operesheni nyingine.

Aidha, uwezo wa ndege hizo kutawanywa katika maeneo mbalimbali unatajwa kuwa faida kubwa kwa Ukraine, kwani utasaidia kupunguza hatari ya kushambuliwa kwa urahisi kwenye vituo vya anga na kuongeza uwezo wa kuhimili mashambulizi dhidi ya miundombinu yake ya kijeshi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *