TEHRAN/YEREVAN — Katika hatua inayoashiria mabadiliko makubwa ya kiusalama, taifa la Armenia inaripotiwa kusaini mkataba wa siri wa ununuzi wa silaha wenye thamani ya dola za Marekani milioni 500 na Iran. Kwa mujibu wa ripoti kutoka shirika la habari la Iran International, inayomilikiwa na Saudi Arabia mkataba huo unahusisha ununuzi wa mtambo wa kisasa wa ulinzi wa anga wa Majed, ulioundwa na kutengenezwa nchini Iran.

Makubaliano haya yanatajwa kubeba uzito mkubwa, kwani yanagharimu takriban theluthi moja ya bajeti yote ya ulinzi ya Armenia kwa mwaka 2024, ambayo inasimama kwenye dola bilioni 1.4. Kwa upande mwingine, hatua hii inatoa fursa kwa Iran kurejesha na kuimarisha ushawishi wake wa kijeshi katika ukanda wa Caucasus Kusini.

Wachambuzi wa masuala ya kiusalama wanaeleza kuwa uamuzi huu wa Armenia unachochewa na hofu inayoongezeka ya kiusalama kufuatia mivutano inayoendelea na jirani yake, Azerbaijan. Aidha, hatua hii inachukuliwa kama mbadala baada ya Armenia kuhisi kupungua kwa uungwaji mkono wa kijeshi kutoka kwa mshirika wake wa kihistoria, Urusi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *